Jumanne, 27 Septemba 2016

Granit ameandika ujumbe huu juu ya kaka yake

#UCL- FC Basel vs Arsenal, Granit ameandika ujumbe huu juu ya kaka yake

Image result for xhaka
Arsenal watakuwa wenyeji wa FC Basel kesho katika mchezo wa Kundi A wa Ligi ya Mabingwa Ulaya utakaofanyika kunako Uwanja wa Emirates.
Mchezo huu utakuwa na msisimko wa aina yake kutokana rekodi nzuri ya FC Basel dhidi ya timu za England, vile vile morali ya Arsenal baada ya kuwa na mwenendo mzuri kwenye michezo ya EPL hasa baada ya kuwanyuka mahasimu wao Chelsea mabao 3-0 mwisho mwa wiki iliyopita.
Msisimko zaidi unakuja pale ndugu wawili wa damu Granit Xhaka anayekipiga Arsenal na Taulant Xhaka anayekipiga Basel.
Vijana hawa waliwahi kucheza pamoja kwenye akademi ya Basel wakati wakiwa wadogo kabisa lakini leo hii wanaenda kukutana wakiwa wakubwa na kila mmoja akicheza timu nyingine.
Hii si mara ya kwanza kwa wawili hawa kukutana kwani awali walikutana kwenye Michuano ya Euro 2016 iliyofanyika nchini Ufaransa, Granit akichezea Uswisi na Taulant akichezea Albania
Hivyo, kuelekea mchezo huu, kupitia akaunti yake ya Instagram, Granit Xhaka ameandika ujumbe wenye safari ya kisoka kati ya kaka yake na yeye mwenyewe.

0 comments:

Chapisha Maoni