Alhamisi, 8 Mei 2014

Mwanamke Azalia kwenye ndoo na kukitupa kichanga chooni.....Polisi wamtia pingu na kumtupa nyuma ya Nondo



MWANAMKE aliyejulikana kwa jina la Hadija Mohammed, mkazi wa Mchikichini, Ilala jijini Dar es Salaam amekumbana na mkono wa sheria baada ya kufanya kitendo cha kinyama kufuatia kujifungulia kwenye ndoo kisha kichanga kukitupa chooni.



Kwa mujibu wa chanzo, mwanamke huyo alikuwa na ujauzito uliotimiza miezi tisa na kila mtu alikuwa akiuona, lakini ghafla siku ya tukio baadhi ya ndugu waligundua kuwa hakuwa na ujauzito tena!
 
NDUGU WAMBANA
Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kuwa baadhi ya ndugu na majirani walipomuona bila ujauzito walimbana kwa kumuuliza iliko mimba hiyo.

“Ndugu zake na majirani walipomuona hana tumbo kama mwanzo walishangaa, wakaamua kumbana tena kwa vitisho kwamba watampeleka polisi.
 
“Ndipo alipoamua kueleza ukweli kwamba, alijifungulia kwenye ndoo lakini mtoto alikwenda kumtupa chooni,” kilisema chanzo hicho.
 
POLISI WAAMBIWA, WAKOMAA NAYE
Habari zilizidi kudai kuwa baada ya majirani na ndugu kuambiwa hivyo walikwenda kutoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Pangani kilichopo Ilala, Dar ambapo walifika na kukiokoa kichanga hicho lakini walikuta kimeshakata roho.
 
MAMA APELEKWA POLISI
Mpashaji wetu alizidi kudai kuwa, baada ya polisi kuuchukua mwili wa mtoto huyo hawakumwacha mama mtu aendelee kuponda maisha uraiani, walimbeba mpaka kituoni hapo na kumfungulia jalada lenye namba ILA/RB/1715/2014 kisha kumpeleka  kwenye Mahabusu ya Polisi Msimbazi huku mwili wa mtoto huyo ukipelekwa Hospitali  ya Amana na baadaye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

NI FUNDISHO
Afande mmoja ambaye aliomba jina lake lisiandikwe, alisema ni lazima Hadija apambane na mkono wa sheria ili iwe fundisho kwa wanawake wengine wenye mchezo huo.
 
“Hii tabia imekua sana. Wanawake wengi wanajifungua kisha wanawatupa watoto chooni au kokote kusikojulikana ili wao waendelee kula raha mjini. Huyu lazima sheria ishike makali yake ili iwe fundisho,” alisema afande huyo. 

0 comments:

Chapisha Maoni