Ijumaa, 6 Juni 2014

H Baba alazwa Muhimbili baada ya kuugua Dengue




Mwimbaji wa bongo Flava, H Baba amelazwa hostpitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya madaktari kugundua kuwa ana ugonjwa wa dengue ambao umeshawauguza watu mbalimbali.
 
H Baba alipelekwa hospitalini hapo jana usiku, na inaelezwa kuwa alianza kujisikia anaumwa tangu Jumatano (June 5), wakati anajiandaa kwenda kuuaga mwili wa marehemu George Tyson aliyefariki kwa ajali ya gari.
 
“Dengue, Muhimbili now saa nane hii, usiku hali ilikuwa mbaya zaidi imebidi tuletwe Muhimbili Hospital.amegundulika ni dengue. thanx to god anaendelea vizuri and that is the last drip.asante my manager Yahya for your greatest help.mungu akuzidishie.asanteni pia my fans kwa maombi yenu.” Amesema mke wa H Baba, Flora Mvungi.

0 comments:

Chapisha Maoni