Jumamosi, 26 Aprili 2014

TAIFA STARS YALAZWA 3-0 NA BURUNDI


April 26, 2014
DSC_0628
Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars imechapwa mabao 3-0 dhidi ya Burundi katika mechi ya kirafiki ya kuadhimisha miaka 50 ya muungano,  uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam.
Mmechi hiyo imechezeshwa na refa Anthony Ogwayo kutoka Kenya akisaidiwa na Gilbert Cheruiyot na Oliver Odhiambo wote pia kutoka Kenya.
Mwamuzi wa mezani alikuwa Israel Mujuni wa Tanzania wakati Kamishna ni Charles Ndagala.
Mabao ya Burundi yamefungwa na Didier Kavumbagu, Amis Twambwe wanaocheza soka la kulipwa nchini Tanzania.
Bao la tatu la Burundi limefungwa na Yufuf Ndikumana na kuifanya Stars iwahuzunishe watanzania waliokuwa na furaha ya kuadhimisha miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

0 comments:

Chapisha Maoni