Ijumaa, 15 Agosti 2014

JINI KABULA: PIGA UA BUSHOKE ANANIOA



Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amefunguka kuwa licha ya penzi lake na msanii Maximilian Bushoke kuwa na sarakasi nyingi lakini anaamini atamuoa.

Akizungumza na paparazi wetu, Jini alisema watu wengi wamekuwa wakiuponda uhusiano wake kwa kuwa Bushoke anaishi Afrika Kusini na kuona hakuna mapenzi ya kweli lakini ukweli anaoujua yeye ndoa ipo.
Msanii wa Bongo Fleva Maximilian Bushoke.
“Piga ua garagaza, Bushoke ndiye mwanaume ambaye anajua kunipa tiba nzuri ya mapenzi, hakuna mwingine, atanioa tu kwa sababu sioni kipingamizi,” alisema Jini Kabula.

0 comments:

Chapisha Maoni