Ijumaa, 15 Agosti 2014

KEYSHIA COLE ADAIWA NI MSAGAJI....VIDEO YAKE MPYA YAZUA UTATA



Keyshia  Cole  ambaye  hivi  karibuni  amepigana  chini  na  mume  wake  Daniel Gibson 'Boobie', mwishoni  mwa  wiki jana  aliachia  video  yake  mpya  ya  wimbo  wa  She, ambayo  ilishangaza  wengi  kutokana  na  kuwamo  matukio  ya  muonekano   wa  kushabikia  mahusiano  ya  kimapenzi  ya  jinsia  moja ( Usagaji )
Katika  video  hiyo, Keyshia  Cole  anaonekana  akimchezea  kimahaba  msichana  mwenzake  anayeonekana  kufanana  naye  kwa  sura, huku  wakiwa  chumbani, jambo  lilioonekana  kama  kuashiria  aina  yake  mpya  ya  mahusiano  ya  kimapenzi  hasa  kutokana  na  kuachana  na  mumewe  siku  chache  zilizopita....

Hata  hivyo, Keyshia  Cole  amejitetea  kuwa  wimbo  huo  uliotayarishwa  na  DJ Mustard  hauhusu  uhusiano  wa  kimapenzi  kati  ya  mwanamke  na  mwanamke.
"Ni  wimbo  wa  kimapenzi, lakini  hauhusu  mapenzi  ya  mwanamke  na  mwanamke  kama  inavyodhaniwa," amejitetea  Keyshia Cole

0 comments:

Chapisha Maoni