Ijumaa, 15 Agosti 2014

RAYUU AOMBA RADHI KWA PICHA ZAKE ZA UCHI......"NAIOMBA RADHI FAMILIA YANGU KWA YOTE NILIYOFANYA"




Msanii  anayefanya  vizuri  kunako  tasnia  ya  filamu  Bongo, Rayuu  Bagenzi  'Rayuu'  ambaye  amewahi  kukumbwa  na  skendo  kibao  ikiwemo  kupiga  picha  za  nusu  uchi  pamoja  na  kuonyesha  michoro  ya  tatoo  katika  sehemu  zake  nyeti  amedai  kuwa  amelazimika  kubadili  mwenendo  wake  hivyo  kuomba  radhi  kwa  kuikwaza  Familia  yake, ndugu, jamaa  na  marafiki
Rayuu  aliamua  kuchukua  maamuzi  hayo  baada  ya  kuona  anakoelekea  si  kwema  hasa  katika  kujenga  msingi  wa  maisha  yake  na  sanaa  kwa  ujumla.....Hata  hivyo  msanii  huyo  alikana  kusambaza  picha  zake  za  utupu  na  kushikilia  msimamo  kuwa  picha  hizo  zilivujishwa  na  watu  wake  waliokuwa  na  nia  ya  kumchafua....

"Naiomba  radhi  familia  yangu, ndugu, jamaa  na  marafiki  pamoja  na  jamii  nzima  kwa  yote niliyofanya.Nimeamua  kubadilika  na  kujitenga  na  watu  wabaya  ambao  hawanitakii  mema. Mimi  ni  mtu  mzima  hivyo  najua  haya  ninayoyafanya  yatakuja  kunigharimu  baadae,"alisema  Rayuu.

Aliongeza  kuwa  skendo  nyingi  chafu  zilimdhalilisha  na  kuleta  fedheha  katika  familia  yake  na  kwamba  hahitaji  tena  kutokea  kwa  hali  hiyo

0 comments:

Chapisha Maoni