Jumatano, 7 Mei 2014


Mwanamke ni mama mwenye nguvu unajua kwa nini kwa sababu mwanamke alitoka katika ubavu wa mwanaume baada ya Mungu kufanya yafuatayo kwa mwanaume
A. Alimpa usingizi mwanaume
B. Alimfanyia upasuaji
C. Damu ilitoka kwa wingi kwa mwanaume
D. Nyama ilitolewa kwa mwanaume
E. Mfupa ulitolewa kwa mwanaume
F. Baada ya kufanyiwa hivyo mwanaume ndipo mwanamke akaumbwa akatoka mwanaume akakiri na kusema huyo ni mfupa katika mfupa wangu na nyama katika nyama yangu –hivyo ataitwa mwanamke napenda ujue kuwa Mwanamke amebeba uponyaji wa mwanaume na mwanaume amebeba vidonda kwa ajili ya mwanamke
Mwanamke ni mfupa mwanaume ni udongo hivyo mwanamke ni:
1. Ni nguvu ya mwanaume
2. Ni jasiri
3. Mchapakazi
4. Mwenye kujiamini
5. Tegemeo la familia
6. Mwalimu wa watoto na familia yake kiujumla
7. Mlinzi wa mwanaume – Bwana akisema ‘’nimefanya jambo jipya duniani mwamke atamlinda mwanaume
8. Chanzo cha baraka ya familia ( nitabariki Uzao wa tumbo lako)
9. Adui wa maadui wa familia (Uzao wa mwanamke utamponda kichwa nyoka na uzao wa nyoka (shetani ) utamponda kisigino (mwanzo)
10. Sauti ya familia (Bwana akamwambia Ibrahimu msikilize mkeo (mwanzo
11. Mponyaji wa familia yake na taifa
12. Mlezi wa huduma (wakamtumikia Yesu kwa mali zao(Luka8.3-4)
13. Mkombozi wa familia na taifa (kupitia mariamu mkombozi Yesu kristo alizaliwa (Luka i.29-35
14. Msaidizi wa Mungu tumfanyie msaidizi wa kufanana naye (mwanzo 2:18)
15. Mwombezi wa familia,huduma na taifa (Tuwapate wapi wa mama waombolezaji
16. Mficha siri wa Mungu (Rebbeca alificha ni nani atayekuwa mtawala kati ya watoto wake wawili Esau na Yakobo.Baada ya kujua umuhimu wa mwanamke tunatakiwa kuangalia kiundani sana tabia 30 za mwanamke bora sio bora mwanamke tumeumia sana baada ya kuowa watu wasio sahihi katika eneo lilosahihi mwanamke bora ni mwamuzi wa familia ndio mleta mabadiliko katika familia mwanamke anayejua kwanini nipo hapa na ninafanya nini?
Mimi nimefanya utafiki kutokana na vitabu na maisha yanayotuzunguka nimeweza kugundua tabia 30 za Mwanamke anayeweza kunifaa mimi na wewe rafiki yangu tuziangalie kwa makini sana na kwa utafiki wa ndani:-
1. Moyo wa Mwanaume humwamini:
Moyo wa M wanaume humwanini Mwanamke bora sio bora Mwanamke, Mwanamke bora hujitahidi sana ili aweze kuaminika kwa mume wake maana Imani ni kitu muhimu sana katika mahusiano, mahusiano yakipoteza Imani hapo hakuna mahusiano, Mwanamke ana uwezo mkubwa sana wa kujiaminisha kwa Mwanaume kuwa yeye ni mtu sahihi na chaguo sahihi kwa Mwanaume wake. Moyo ndio unaothibitisha kuwa huyu ni mtu sahihi au sio sahihi
Moyo ndio unamkubari mtu
Moyo ndio sauti ya mwisho
Moyo ndio chanzo cha upendo
Moyo ndio jibu la maisha yako ya mapendo
Moyo ndio chemichemi ya mapenzi
Moyo ndio unaoamini na kinywa husema yaliyo maamuzi ya moyo.
Huyu Mwanamke anatakiwa awe na jibu kwa Mwanaume- Upendo wa kweli hautambuliki kwa muonekano wa mtu bali upendo huambulika toka moyoni:- Hivyo Mwanamke bora ni Yule anayeweza kuushika moyo wa Mwanaume na kujiaminisha kwake.
2. Huondoa umaskini
Mwanamke bora katika maisha yako ni Yule mwenye mawazo mazuri ya kuondoa umaskini katika maisha yako- hana wazo baya, wengi wao wanatamani kuolewa ili awe na sifa mtaani kuwa ameolewa lakini ni tegemezi, hana wazo jipya la kubadilisha maisha yako. Hawa sio wanawake sahihi mawazo yake yanamtegemea mwanaume, wazo lake ni kuzaa watoto hana wazo la maendeleo, hajui maumivu ya maisha huwa wanarudisha nyuma ndoto zako kutokutimia kwa wakati wake. Mwanamke bora ni Yule mwenye mawazo ya maendeleo, mwenye hasira na umaskini mpenda mafanikio huyo ndiyo anafaa kuolewa
3. Kamwe hamtendei Mume wake mabaya
Mwanamke bora yaani niniamaanisha aliye sahihi ni Yule mwenye moyo safi kwa mume wake,
1. Hawazi mabaya bali mema kwa mume wake,
2. Hawezi kumtendea mume wake mabaya,
3. Hawezi kumuumiza mume wake,
4. Hawezi kumtonesha vidonda mume wake,
5. Hawezi kuumsaliti mume wake,
6. Hawezi kumtendea yasiyo haki mume wake,
7. Hawezi kumchafua mume wake na kumdharirirsha katika jamiii iliyowazunguka,
8. Hawezikumtukana Mume wake,
9. Hawezi kushabikia maumivu na mateso ya Mume wake,
10. Hawezi kuwa radhi na maadui wa Mume wake,
11. Hawezi kuwa jeuri kwa Mume wake,
12. Hawezi kumtendea Mume wake mabaya.
13. Amejaa heshima kwa Mume wake,
14. Adabu,
15. Utu wema anatunza uthamani wa Mume wake
16. Amejaa utiifu na upole kwa Mume wake
17. Amejaa unyenyekevu na uaminifu kwa Mume wake,
18. Amejaa amani na furaha ya kweli kwa Mume wake-
19. Anayeshinda uovu kwa wema,
20. Mwenye upendo wa kweli kwa mume wake. Huyu ndiye Mwanamke unayeweza kumuowa au kuishi naye na ndio sifa ya Mwanamke anayehitajika katika maisha yako. Mwanamke huyu ataheshimika na kuthaminiwa na watu na hatakosa upendo wa dhati kutoka kwa Mume wake.

0 comments:

Chapisha Maoni